Tuesday , 3rd May , 2022

Mtoto wa kiume wa mbunge maalum nchini Kenya David Ole Sankok, aitwaye Memusi Sankok mwenye umri wa miaka 15, amejipiga risasi kwa kutumia bastola ya baba yake nyumbani kwao katika eneo la Ewaso Nyiro, kaunti ndogo ya Narok Kusini.

Bastola

Imeelezwa kwamba tukio hilo limetokea jana Mei 2, 2022, majira ya mchana, baada ya mtoto huyo kuchukua bastola hiyo iliyokuwa imefichwa kwenye sanduku salama mara tu baba yake alipoondoka nyumbani baada ya kumhoji kwanini hakwenda shule licha ya kupewa pesa.

Memusi alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne, katika Shule ya Upili ya Kericho, na polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini sababu iliyopelekea mtoto huyo kujitoa uhai.