Ochieng hakuwahi kusomea ufundi wa magari
Kijana mmoja kutoka Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya anayetambulika kwa jina la Bernard Otieno Ochieng, ameshangaza watu kutokana na kipaji chake na uwezo wa ubunifu baada ya kubuni gari lake la siti mbili za kukaa.
Mwaka 2010, Ochieng aliacha shule baada ya kushindwa kulipa karo, baada ya hapo alianza kujifunza ufundi wa magari kwa sababu ni kitu ambacho alikuwa anakipenda tangu akiwa shule. Kipindi yupo shule alikuwa anapenda kutumia computer kuangalia mtandaoni jinsi magari yanavyoundwa na kujifunza.