
Baadhi ya silaha walizokuwa nazo majambazi hao
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo Jumanne Muliro, na kusema watuhumiwa hao wa ujambazi walijihami kwa silaha na kuanza kuwashambulia askari kwa risasi na ndipo walipodhibitiwa.
Kamanda Muliro amesema baada ya kupekuliwa watuhumiwa hao, walikutwa na bastola moja iliyofutwa namba, silaha za jadi mapanga manne na funguo nyingi aina mbalimbali za kufungulia magodown na ofisi za kiwanda hicho, gari No. T 201 DXN HIACE ikiwa tayari imemekwisha pakiwa mali za wizi box zaidi ya 70 za vipuri.