Tuesday , 2nd Aug , 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kwamba wamekubaliana na Rais wa Zambia Hakaiende Hichilema, kurejesha undugu ulioasisiwa na waasisi wa mataifa hayo mawili Hayati Nyerere na Hayati Kaunda.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Rais wa Zambia Hakainde Hichilema

Kauli hiyo ameitoa hii leo Agosti 2, 2022, jijini Dar es Salaam, mara baada ya kumaliza mazungumzo ya faragha na mgeni wake Rais wa Zambia Hakainde Hichilema, Ikulu ya Dar es Salaam.

"Tumekubaliana na ndugu yangu Hichilema kwamba turudi turudishe ule undugu kama tulivyoachwa na wazazi wetu, tumeangalia uhusiano wa kisiasa nchi zetu kwa yoyote yaliyotokea lakini lazima turudi sisi kama viongozi wa nchi tuwaongoze watu wetu waelewane vizuri," amesema Rais Samia 

Tazama video hapa chini