Thursday , 1st Sep , 2022

Moto umeteketeza nyumba yenye vyumba sita hii leo Septemba Mosi, 2022, eneo la Kata ya Chamwino Chinangali Jijini Dodoma, na kuunguza vitu vyote vilivyomo ndani ya nyumba hiyo, huku chanzo kikitajwa kuwa ni kuvuja kwa gesi ambayo hewa yake ilikutana na joto la mkaa.

Nyumba iliyoungua

Akizungumza katika eneo la tukio Afisa Oparesheni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Dodoma, Inspekta Deugratius Inano, amesema chanzo cha moto huo ni kuvuja kwa gesi ambayo hewa yake ilikutana na joto la mkaa.

Akizungumza kwa niaba ya familia iliyounguliwa nyumba Robert Mwalugeni, ameeleza alichokiona kabla ya moto kutokea.