Monday , 3rd Oct , 2022

Takribani ndege milioni 48 wameteketezwa nchini Uingereza na Umoja wa ulaya mwaka jana pekee kutokana na mlipuko wa homa ya mafua ya avian.

Uingereza pekee kesi 161 za ugonjwa huo hatari wa mafua ya (HPAI) ziligundulika kwenye mifugo jamii ya ndege na kupelekea kuteketeza mifugo milioni 3.2 .

Hiyo inakua ni rekodi kubwa kulinganisha na ya awali ya mwaka  2020/21 ambapo kulikua na kesi 26 pekee.   

Serikali Ya Uingereza imesema kwamba ndege walioteketezwa ni idadi ndogo sana ya ndege milioni 20 kwa wiki .

Homa ya mafua ya Avian imesharipoti visa  1,727 katika aina 59 za tofauti za jamii ya ndege.