Wednesday , 5th Oct , 2022

Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amewaomba msamaha Wakenya kufuatia mtafaruko uliosababishwa na mtoto wake, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, kupitia ukurasa wake wa Twitter kwa kuandika ujumbe wa kwamba yeye na jeshi lake wanaweza kuliteka Jiji la Nairobi kwa wiki mbili tu.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni

Aidha katika barua yake aliyoiandika hii leo Oktoba 5, 2022, Rais Museveni pia, amewaomba msamaha wanajumuiya wa Afrika Mashariki pamoja na raia wa Uganda ambao walikerwa na maandiko ya Jenerali Kainerugaba kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Akizungumzia hatua za kumpandisha cheo kutoka kuwa Luteni Jenerali hadi kuwa Jenerali kamili, Rais Museveni amesema hatua hiyo ilikuja kutokana na yeye kutenda kosa moja tu ukilinganisha na mema mengi aliyoyafanya na atakayoendelea kuyafanya.