Friday , 7th Oct , 2022

Viongozi kutoka Ukraine, Uingereza na Uturuki wamejiunga leo na wenzao wa Umoja wa Ulaya kwa mkutano wa kwanza wa kilele unaofahamika kama Jumuiya ya Kisiasa ya Ulaya.

Unalenga kulileta pamoja bara la Ulaya katika wakati ambao Urusi inaendesha vita dhidi ya Ukraine. Mkutano huo unaofanyika mjini Prague, ukiwa ni wazo la Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron,

Umoja wa Ulaya kuwa ni jukwaa la uratibu wa kisiasa kwa mataifa 44 yanayohudhuria. Macron amesema unatuma ujume wa umoja.

Urusi ambayo haijaalikwa, imeugubika mkutano huo wakati mazungumzo yakilenga msukosuko wa kiuchumi na usalama kutokana na uvamizi wake wa jirani yake anayeegemea nchi za Magharibi.