Saturday , 8th Oct , 2022

Watu wawili  waliotambulika  kwa majina ya  Baraka Mollell na Enock  Lembris wamefariki na mmoja akijeruhiwa  baada ya kuangukiwa na kifusi  katika machimbo ya moramu ya mgodi wa Ngurumausi uliopo katika kata ya Muivaro jijini Arusha.

Mwenyekiti mtaa wa Ngurumausi Jonas Jackson anabainisha  kuwa ajali hiyo imetokea  wakati ambapo vijana hao waliofariki walikuwa wanafanya shughuli za upakiaji katika machimbo hayo ya Moramo na kwambwa walikuwa wamejipumzisha ndipo wakafukiwa na kifusi.

Diwani wa Kata ya Mwivaro Philemoni Mollel amewataka wachimbaji wa mgodi huo kutopumzika katika maeneo hayo mara baada ya kazi kwa kuwa sio salama kwa Maisha yao.

Baadhi ya wakazi wa maeneo hayo wameiomba serikali kuweka miundombinu itakayosaidia shughuli za uchimbaji ili kuepusha madhara yanayotokea mara kwa mara.

Miezi Kadhaa nyuma mgodi huu ulifungwa na mkuu wa wilaya ya Arusha Saidi Mtanda mara baada ya watu wengine kufariki kwa kufukiwa na kifusi.