Tuesday , 25th Oct , 2022

Waziri Mkuu mpya wa Uingereza Rishi Sunak amekutana na Mfalme Charles III na kuruhusiwa kuanza safari ya kuunda serikali yake 

Katika hotuba yake ya kwanza kama waziri mkuu Sunak anasema daima atamshukuru Boris Johnson kwa mafanikio makubwa katika utawala wake huku akisisitiza kuwa serikali yake itakuwa na uadilifu, weledi na uwajibikaji 

Sunak ameeleza kuwa katika utawala wake anakwenda kuliunganisha taifa hilo na sio kwa maneno tu lakini kwa vitendo huku akieleza kuwa anakwenda kufanya maamuzi magumu kwa faida ya taifa hilo

"Nitajaribu kurekebisha makosa yaliyofanywa na mtangulizi wangu, kurejesha imani katika siasa lakini na kutakuwa na maamuzi magumu mbeleni" amesema Sunak