Friday , 28th Oct , 2022

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Rashid Chuachua ametoa muda wa siku tano kwa wananchi waliovamia msitu wa Mlima Mbeya kuondoka mara moja  kabla serikali haijachukua hatua za kisheria.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dk. Rashid Chuachua

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Rashid Chuachua ametoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa Kijiji cha Ihombe baada ya kuripotiwa matukio ya uchomaji kwenye msitu unaomilikiwa na Wakala wa Huduma za Misitu nchini TSF.

Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Wilaya ya Mbeya, Eunice Mbilinyi amewataka wananchi kuacha kujihusisha na shughuli za kibinadamu kwemye hifadhi za misitu.