Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Mwanaume anaridhikaje na mke mmoja"- Musa

Wednesday , 28th Dec , 2022

Musa Hasahya ni mkulima kutoka Butaleja nchini Uganda ambaye ana wake 12, watoto 102 na wajukuu 568 amesema kwamba hatoongeza tena ukubwa wa familia yake kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Musa akiwa na watoto wake

Musa ameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuwataka wake zake kuanza kutumia uzazi wa mpango ili familia iweze kununua mahitaji ya chakula yatakayokidhi familia.

"Kipato changu kimekuwa kikishuka chini kutokana na kupanda kwa gharama za maisha na familia yangu imekuwa kubwa na kubwa zaidi, nilioa mwanamke mmoja baada ya mwingine, mwanaume anawezaje kuridhika na mwanamke mmoja," amesema Musa

Kuoa wake wengi ni halali nchini Uganda, lakini wake zake wote wanakaa kwenye nyumba moja ili kuwazuia wasiweze kutoroka na wanaume wengine.

Aidha Musa hawezi tena kufanya kazi kwa sababu ya afya yake kuzorota kutokana na maradhi na wake zake wawili wameondoka kutokana na changamoto za kifedha.

Zulaika, mke wake mdogo na mama wa watoto wake 11, amesema, "Sina watoto tena, nimeona hali mbaya ya kifedha na sasa natumia tembe (vidonge) ya kupanga uzazi, Lakini dawa za kupanga uzazi ni mwiko nchini, kwani mara nyingi zinahusishwa na uasherati,".

Umri wa watoto wa Musa ni kati ya miaka sita hadi 51, na takriban theluthi moja ya watoto wake wanaishi na Musa nyumbani kwake.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava