
Wananchi wa Manispaa ya Bukoba
Akizungumza wakati wa kuzindua mradi huo katika Kata ya Ijuganyondo iliyoko katika manispaa ya Bukoba, Naibu Waziri wa Nishati Stephen Byabato, amesema kuwa miradi yote iliyoko chini ya REA haina utaratibu wa kulipa fidia, na kwamba wanaotekeleza mradi huo wanafahamu kuwa kuna mazao ya wananchi katika mashamba hivyo watatumia busara wakati wa utekelezaji.
"Nimeamua kulisema hili hapa kwa sababu ni mradi wa kwanza wa aina hii kwenu huko vijijini wanalijua hili, niwaombe viongozi wakiwamo wenyeviti wa serikali za mitaa, madiwani na vyama vya siasa wa maeneo ambayo mradi huu utapita, kukaa vikao na wananchi na kufanya mikutano ya haraka, ili kukubaliana na mkandarasi wapi wapitishe laini za umeme" amesema Byabato
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa REA Tanzania Mhandisi Hassan Said, amesema kuwa wao pamoja na kwamba jukumu lao ni kupeleka umeme vijijini, lakini walifikia uamuzi wa kuwahudumia pia wananchi wanaoishi pembezoni mwa miji, manispaa na majiji, kutokana na maeneo hayo kuwa na watu ambao maisha yao hayana tofauti na wanaoishi vijijini.