Ndege ya majaribio
DC Mboni ametoa kauli hiyo hii leo Februari 13, 2023, wakati akizungumza na East Africa TV & East Africa Radio Digital, mara baada ya taarifa kusambaa mitandaoni zikionesha kwamba kuna ajali ya ndege imetokea na kuua watu wapatao 10, majeruhi 23 na walionusurika ni 9.
"Lilikuwa ni zoezi la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ambalo huwa wanalifanya kila baada ya miaka miwili kuweza kujipima utayari wa kuokoa iwapo itatokea dharura ya aina yoyote, hili zoezi ili liende sawia lazima waweke scenario, kiuhalisia hakuna vifo vilivyotokea wala majeruhi," amesema DC Mboni Mhita.
Tazama video hapa chini

