Aidha wanafunzi hao wamepatiwa elimu ya Afya huku Rais wa Club hiyo Krutin Shah akisema kuwa utoaji wa elimu na matibabu bure ni moja ya mikakati yao ya kukabiliana na magonjwa tangu walipoanzisha kambi za matibabu mwaka 2012.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kerege, Esther Awino amewaomba wazazi kushirikiana na walimu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakumba wanafunzi ili waweze kusoma katika misingi bora.
Nao baadhi ya wazazi wamesema kuwa matibabu hayo yamewasaidia kwa kiasi kikubwa kwani wameweza kujua afya za watoto wao na kuwataka wazazi wengine kuhakikisha wanawapeleka watoto kujua afya zao.



