Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu watokwa damu, Figo zafeli na watano wafariki

Thursday , 16th Mar , 2023

Wizara ya Afya imesema inafuatilia ugonjwa usiojulikana uliotokea mkoani Kagera wilaya ya Bukoba vijijini ambapo watu saba walipata dalili za homa, kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya miili yao na Figo kushindwa kufanya kazi, ambapo watano wamefariki dunia na wawili wako hospitali.

Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu,

Wizara ya imesema inafuatilia ugonjwa usiojulikana uliotokea mkoani Kagera na kuua watu watano baada ya watu saba kupata dalili za homa, kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya miili yao na Figo kushindwa kufanya kazi, ambapo wawili wako hospitali.

Taarifa hiyo imetolewa leo Machi 16, 2023, na Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu, na kusema Ugonjwa huo usiojulikana umetokea wilaya ya Bukoba vijijini katika vijiji vya Bulinda na Butayaibega, ambapo inasadikiwa watu hao saba walipata dalili hizo za homa.

"Serikali imechukua hatua za kudhibiti ugonjwa huo ili usisambae kwa kuchukua sampuli kutoka kwa wagonjwa na waliofariki ili kubaini chanzo cha ugonjwa huo na ufuatiliaji wa watu wenye viashiria vya ugonjwa kwenye jamii," amesema Profesa Nagu.

Aidha Profesa Nagu ameongeza, "Pia dawa, vifaa na vifaa tiba muhimu vipo katika vituo vya kutolea huduma za afya mkoani Kagera na wagonjwa wanaendelea na matibabu, na elimu ya afya inaendelea kutolewa kwa jamii mkoani Kagera ili kuchukua tahadhari,"- Profesa Tumaini Nagu, Mganga Mkuu wa Serikali

Katika hatua nyingine Wizara ya Afya imewatoa hofu Watanzania kuhusu ugonjwa huo na kushauri, "Mtu yeyote mwenye dalili za homa, kutapika, kuharisha, kutoka damu na mwili kuishiwa nguvu anashauriwa kuwa kituo cha kutolea huduma za afya, kuepuka kumgusa mgonjwa au majimaji ya mwili, mate, machozi, damu, mkojo na kinyesi kitokacho kwa mgonjwa au yeyote mwenye dalili hizo,".
 

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya