Thursday , 8th Feb , 2024

The African Princess Nandy amefunguka baada ya kupokea ujumbe Instagram kutoka kwa staa wa muziki duniani #UsherRaymond akitaka kufanya naye kazi.

Picha ya Nandy na Usher Raymond

“Najisikia furaha na nimetoboa, tulikuwa tupo studio ndio tulionea hapo na Management yote iliyokuwa hapo imeona. Hii ndio mara ya kwanza sijawahi kuwasiliana naye au kuwaza kum-DM kuomba kufanya naye kazi”. amesema Nandy

Pia ameongeza kusema tayari anajiaanda na safari ya kwenda Marekani kwa ajili ya kufanya naye wimbo huo.