Wednesday , 14th May , 2025

Rais wa zamani wa Uruguay José Mujica, anayejulikana kama "Pepe", amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 89.

Rais wa zamani wa Uruguay José Mujica, anayejulikana kama "Pepe", amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 89.

 

Mpiganaji huyo wa zamani ambaye alitawala Uruguay kuanzia 2010 hadi 2015 alijulikana kama "rais maskini zaidi" kwa sababu ya maisha yake ya kawaida.

 

Rais wa sasa Yamandu Orsi alitangaza kifo cha mtangulizi wake kwenye jukwaa la X: "asante kwa kila kitu ulichotupa na kwa upendo wako mkubwa kwa watu wako."

 

Chanzo cha kifo cha mwanasiasa huyo hakijajulikana lakini alikuwa akiugua saratani ya umio.