Tuesday , 10th Jun , 2025

The African Princess Nandy amefunguka kuwa linapokuja suala la Mapenzi/Mahusiano hawezi kumshauri kitu chochote msanii mwenzie Zuchu ,mbali na hilo pia bado ameendelea kukazia suala la pete yake kupotea huku akisema kuwa atakaye ipata atapewa zawadi ya milioni kumi

Pichani Nandy na Zuchu

"Kiukweli siwezi kumshauri Zuchu kwenye mitandao kwasababu tunashauriana vitu vingi sana ushauri wangu mwingi na wake ninao mwingi kuhusu ndoa hata kwangu ilikuwa kama surprise lakini kwenye shughuli nitakuwepo" Amesema Nandy

"Bado sijapata pete yangu na nisingekuwa na Billnass wakati inapotea shida ingekuwa kubwa sana na Mungu alinisaidia,Atakaye niletea (Pete) nitampatia milioni 10 sio kwasababu inauzwa zaidi ya hapo bali ina memory kubwa kuliko wanavyodhania'' Amesema Nandy