Monday , 7th Jul , 2025

Siyo kila mvumbuzi alifurahia kazi ya mikono yake, baadhi ya wavumbuzi wakubwa duniani waliishia kuishi na huzuni kwa sababu ya jinsi uvumbuzi wao ulivyotumika kinyume na matarajio yao.

Hii hapa ni orodha ya waliowahi kujutia kazi zao:

1. Oppenheimer – Baba wa bomu la atomiki. Baadaye akajuta kwa mauaji na uharibifu wa Hiroshima & Nagasaki mwaka 1945.

2. Kalashnikov – Aliunda AK-47 kwa ulinzi wa taifa, lakini alihuzunika ilipotumika kwenye mauaji ya raia.

3. Philo Farnsworth – Mvumbuzi wa luninga, alikasirishwa kuona TV ikigeuzwa burudani tupu badala ya kufanyika kuwa sehemu ya kutoa elimu kama ilivyokuwa lengo lake.

4. Ethan Zuckerman – Mtengenezaji wa Pop-up Ads, alikuja kuomba msamaha hadharani kwa “usumbufu” aliouleta mtandaoni.  (Pop-up Ads - matangazo yanayokuja wakati unaperuzi kwenye wavuti mbalimbali)

5. Anna Jarvis – Alianzisha Mother’s Day kwa upendo, lakini alijuta ilipochukuliwa na wafanyabiashara kama fursa ya kuuza kadi & maua tu.

6. Wright Brothers – Walitaka ndege zisaidie usafiri wa watu, lakini zilipoanza kubeba mabomu vitani, Orville alijutia uvumbuzi wao.

Ujumbe mkubwa ‘’Teknolojia si tatizo ni matumizi yake’’