Wanafunzi 11 mbaroni kwa tuhuma za kuchoma moto
Jeshi la Polisi mkoa wa Geita linawashikilia wanafunzi 11 akiwemo msichana mmoja kwa tuhuma za kuchoma moto shule ya sekondari Geita mara tatu tofauti, Julai 5, 6 na 14 huku likidai chanzo cha kufanya hivyo ni upendeleo waliokuwa wanaupata wanafunzi wanaokaa bweni.