Razak Siwa aipaisha Dodoma Jiji
Kocha wa magoli kipa wa klabu ya Yanga, Razak Siwa ameipaisha klabu ya Dodoma Jiji na kusema ni timu nzuri hivyo hawana budi kupambana ili kusaka alama tatu kwenye mchezo wa VPL utakaowakutanisha wawili hao kesho Julai 18, 2021 kwenye dimba la Jamhuri Jijini Dodoma.