Coastal wakanusha, kumfuta kazi kocha Mgunda
Klabu ya Coastal Union ya Tanga kupitia kwa katibu mkuu wake Rashid Mgweno, imekanusha taarifa za kumfuta kazi kocha mkuu wa kikosi hicho Juma Mgunda na imesisitiza kuwa bado wanamipango ya muda mrefu na kocha huyo.