5 wahukumiwa kunyongwa kwa mauaji
Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, iliyofanya kikao chake mkoani Njombe, imewahukumu kunyongwa hadi kufa washtakiwa watano waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji namba 84 ya mwaka 2014, ya Alice Mtokoma (56) mkazi wa kijiji cha Usalule, wilayani Wanging’ombe mkoani humo.