Polisi wasimulia Tembo alivyoteketeza familia ya 3
Watu watatu wa familia moja, mume, mke na mtoto wao, wamepoteza maisha na mwingine mmoja kujeruhiwa, Januari 3, 2021, majira ya saa 11:00 jioni, baada ya kuvamiwa na kushambuliwa na Tembo katika Kijiji cha Nshabaiguru, Kata ya Kihanga wilayani Karagwe, mkoa wa Kagera.