Magufuli aeleza alivyokoshwa na gazeti la Marekani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Dkt. John Magufuli, amesema kuwa ameona takwimu za dunia nzima kuhusu maambukizi ya virusi vya Corona zilizotolewa na gazeti la New York Times la nchini Marekani, ambapo limeonesha kuwa Tanzania haina kabisa maambukizi ya ugonjwa huo.