Chanzo cha moto Mlima Kilimanjaro chatajwa
Kamishna Msaidizi wa Mawasiliano wa TANAPA, Paschal Shelutete, amesema kuwa moto ulioteketeza na unaoendelea kuteketeza sehemu ya hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, ulitokea baada ya nyasi kavu kushika moto kwa bahati mbaya wakati wa zoezi la kupasha chakula cha wageni katika kituo cha Whoma.