RC Gambo kuwasweka rumande wazazi Arusha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, amesema ataanzisha msako wa kuwakamata na kuwaweka rumande wazazi wote, ambao hadi sasa bado hawajawapeleka watoto wao kuripoti shuleni kwa ajili ya kuanza kidato cha kwanza na kwamba dhamana ya mzazi atakapokamatwa itakuwa ni mtoto kuanza shule.