
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo
RC Gambo amesema kuwa licha ya Mkoa huo kufaulisha Jumla ya watoto 35,254, lakini taarifa ya Januari 24, 2020, imeonesha kuwa ni wanafunzi 25,483, ambao ni sawa na asilimia 72 ndio wamewasili katika shule walizopangiwa.
"Kuanzia sasa wanafunzi kokote waliko, wazazi kokote waliko, viongozi wangu wote katika ngazi zote, wataanza msako maalumu wa kuwatafuta wazazi wote ambao watoto wao hawajapelekwa shule na tukimkamata mzazi tutamuweka lock up na dhamana yake ni mtoto kuripoti shuleni" amesema RC Gambo.