Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba (kulia) akitoa hotuba ufunguzi wa kikao kazi cha mwaka kinachowahusisha maafisa wakuu wa jeshi la Polisi na makamanda wa mikoa na vikosi kinachofanyika mkoani Dodoma.
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba amewataka maafisa wa jeshi hilo kutenda haki kutokana na baadhi yao kunyooshewa vidole kwa kukiuka misingi ya kazi zao ikiwamo kujihusisha na rushwa.