Tanzania kushirikiana na Belarus
Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) limesaini rasmi Hati ya Makubaliano (MoU) na Kituo cha Taifa cha Kukuza Mauzo ya Nje (NEPC) cha Jamhuri ya Belarus, ikiwa ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya nchi hizi mbili.

