TFDA kuendelea kukagua vibali vya uingizaji sukari
Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA), imesema inaendelea kusimamia vibali vya uingizaji wa sukari ili kuhakikisha sukari inayoingizwa hapa nchini inakidhi viwango na ni bora kwa matumizi ya binadamu.