Uchumi wa nchi uendane na kipato cha wafanyakazi
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini Tanzania – TUCTA Bw. Nicholous Mgaya, amesema licha ya uchumi wa nchi kukua kwa kiwango cha asilimia 7 kwa mwaka, bado ukuaji huo hauendi sambamba na uboreshaji wa maslahi ya wafanyakazi.