Mke adaiwa kutafuta wauaji waliomuua mumewe
Washtakiwa watano akiwemo mke wa marehemu ambaye inadaiwa alipanga njama za kumuua mume wake aitwaye Mange Washa na aliwalipa wauaji wawili kiasi cha shilingi laki nane, wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza na kusomewa shtaka moja la mauaji.