Uchunguzi wa kina waombwa ufanyike kifo cha Askofu
Vyombo vya dola vimetakiwa kufanya uchunguzi wa kina wa kifo cha Askofu mstaafu Boniface Kwangu, wa kanisa la Anglikana Diocese ya Victoria Nyanza, anayedaiwa kupotea tarehe 28 na mwili wake kukutwa ukielea ndani ya maji kandokando ya Ziwa Victoria karibu na linapojengwa daraja la JPM.