Tembo waanza kufukuzwa kwa Helikopta
Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na utalii, pamoja na vyombo vinavyojihusisha na wanyamapori na uhifadhi nchini, wameanza zoezi la kuwafukuza Tembo kutoka maeneo ya karibu na makazi ya wananchi na kuwaswaga kuelekea maeneo ya mbugani ili wananchi wawe salama.