Kamati ya kuangalia migogoro ya mipaka kuundwa

Mbunge wa Iramba Magharibi ambaye pia ni Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (wa pili kulia) akiwa ameongozana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ,Mhe. Mary Masanja (Mb) (katikati) na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Iramba kukagua eneo la kitalu cha miche ya miti la Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) lililoharibiwa na wananchi katika Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema Serikali itaunda Kamati ya kuangalia migogoro ya mipaka na vijiji vinavyozunguka Msitu wa Hifadhi wa Bonde la Wembere uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida.