Tanzania mbioni kuuza parachichi nchini Marekani
Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amesema kufuatia mahusiano mazuri ya kibiashara baina ya Tanzania na Marekani, Tanzania ipo mbioni kunufaika na soko kubwa la Parachichi nchini Marekani baada ya kukamilika kwa taratibu chache za masuala ya usafi wa mazao