Waliokuwa wanajifungulia chini ya mti waokolewa
Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 300, kwa ajili ya kujenga daraja la mto Mwandoya jimbo la Kisesa, Meatu mkoani Simiyu, ili kunusuru wananchi kusombwa na maji ikiwamo wanawake kujifungulia chini ya mti, kutokana na kushindwa kupita kwenye mto unapokuwa umejaa maji.