Alhamisi , 5th Dec , 2019

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, linawashikiliwa watu 33 kwa tuhuma za wizi wa Mafuta, yanayotumika kuendeshea mitambo katika Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa na mabomba yanayotumika kumwagilia mashamba ya Miwa kiwandani hapo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, ACP Wilbroad Mutafungwa, amesema katika oparesheni waliyoifanya kwa siku za hivi karibuni, wamefakiwa kuwakamata watuhimiwa hao huku akitoa wito kwa wamiliki wa Viwanda pamoja na Makampuni binafsi mkoani hapo, kushirikiana na Jeshi hilo kwa lengo la kutatua ufumbuzi wa changamoto za kiusalama.

"Watu wanne kati yao walikamatwa kwenye Bwawa lile wakiwa wanafanya Uvuvi haramu, tumefanikiwa pia kukamata Makasia 4, Mitumbwi 9 pamoja na Nyavu 6" amesema Kamanda Mutafungwa.

Watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na kwamba upelelezi utakapo kamilika, watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.