Amina Hassan, aliyechomwa visu hadi kuafariki
Baadhi ya majirani wamesema wanandoa hao walikuwa na mgogoro juu ya kukutana kimwili ambapo walishauriwa na daktari wasikutane kwa muda kutokana na changamoto za kiafya zinazowakabili, hivyo mwanaume alikataa ushauri wa daktari na amekuwa akitumia nguvu kumuingilia mkewe.
Majirani wanasema wawili hao walikuwa wametengana vyumba vya kulala kutokana na mwanaume alikataa ushauri wa kutumia dawa walizoashauriwa na madaktari.
Akizungumza kwa machungu mtoto wa marehemu ameelezea mara ya mwisho alivyokuwa anaangalia TV na mama yake mpaka kupitiwa na usingizi na ghafla akashtuka na kumkuta baba yake anampiga na kumchoma na visu mama yake sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo tumboni, chini ya kifua mbavuni na mgongoni mpaka kisu kilipomkatikia mwilini ndiyo akafungua mlango wa nyumba na kukimbia kusikojulikana.

