Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Gervas Ilonda
Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Gervas Ilonda, na kusema sifa za kujiunga ni lazima kijana awe na miaka 18 hadi 26 kwa wenye elimu ya kidato cha nne hadi cha sita na umri usiozidi miaka 27 kwa wenye elimu ya juu pia awe na afya nzuri na akili timamu.
"Awe Mtanzania mwenye tabia na nidhamu nzuri, hajapatikana na hatia ya makosa ya jinai mahakamani na kufungwa, awe na cheti halisi cha kuzaliwa, vyeti vya shule na taaluma, awe hajatumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo, asiwe ameoa au kuolewa" amesema Luteni Kanali Ilonda
Aidha Luteni Kanali Ilonda amesisitiza, "Maombi yote yaandikwe kwa mkono na yawasilishwe makao makuu ya jeshi, Dodoma kuanzia tarehe ya tangazo hili yaani leo hadi tarehe 20 Machi, 2023 yakiambatishwa na nakala ya kitambulisho cha Taifa au namba ya NIDA, nakala ya cheti cha kuzaliwa, vyeti vya shule na chuo, nakala ya cheti cha JKT na namba ya simu ya mkononi ya mwombaji".







