Alhamisi , 1st Aug , 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo Agosti 1, ametengua uteuzi wa  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Vijini Kayombe Rioba baada ya utendaji wake  wa usimamizi wa miradi ya maendeleo kutoridhisha.

Waziri wa TAMISEMI, Seleman Jaffo

Akitoa taarifa hiyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Seleman Jaffo, ameeleza kuwa Mkurugenzi huyo alikuwa hazingatii miongozo na taratibu za manunuzi.

"Imeonekana wazi kwamba Mkurugenzi huyu alinunua sumu ya kupulizia mchwa kwa ajlili ya majengo kwa kiasi cha sh milioni 66,  ni zaidi ya matarajio ya matumizi ya fedha katika eneo hilo'', amesema Waziri Jaffo.

Hivi sasa atakayekaimu nafasi hiyo ya ukurugenzi ni Mhandisi Godfrey Mlowe, ambaye ni Meneja wa TARURA katika Halmashauri hiyo na kwamba atasimamia ukamilishaji wa majengo ya Hospitali pamoja na ujenzi wa vituo vya afya vya Mikese na Kinonko.