
Balozi wa Uholanzi Jaap Frederiks akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu
Balozi huyo ameyasema hayo leo alipokutana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipofika Ikulu kwa lengo la kuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
Makamu wa Rais alimhakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania itazidi kuimarisha uhusiano wake na nchi ya Uholanzi hasa katika sekta ya kilimo, elimu na uboreshwaji wa mazingira ya uwekezaji ili kufikia lengo la Tanzania ya Viwanda.
Mh. Balozi ameahidi kwenda kuwa mjumbe mzuri huko anapoelekea ikiwa ni pamoja na kutangaza vivutio vilivyopo nchini.