Jumanne , 7th Mar , 2023

Watu saba wamefariki dunia na wengine ambao idadi bado haijajulikana kujeruhiwa katika ajali ya gari la Sheraton lililopinduka baada ya tairi la mbele kuchomoka na kuangukia mtaroni, lililokuwa linatokea mkoani Mwanza kwenda Ushirombo wilayani Mbogwe mkoani Geita.

Eneo la ajali

Ajali hiyo imetokea leo Machi 7, 2023 imetokea majira ya saa10:30 jioni katika Kijiji cha Mwilima karibu na mbuga ya Ibanda mpakani mwa mkoa wa Geita na Mwanza.

Na majeruhi wa ajali hiyo wanaendelea kupatiwa huduma katika hospitali ya rufaa mkoa wa Geita na kituo cha afya Kasamwa.

 

Basi lililopata ajali