
Moja ya marekebisho muhimu yaliyofanywa na bunge ni kulitaka jeshi kuweka alama kwenye vyombo vyao vyote na mavazi ili kuvitenganisha na vile vya raia.
Pia, sasa ni sharti kwa mkuu wa mahakama ya kijeshi kuwa wakili katika cheo cha Jaji wa mahakama kuu na kwamba aliyehukumiwa anaweza kukata rufaa katika mahakama ya juu zaidi ya kiraia.
Sheria hii imepingwa na watetezi wa haki za binadamu na upinzani wekisema kwamba itatumika kuwalenga wakati nchi inakaribia uchaguzi ujao.