Alhamisi , 18th Feb , 2016

Mitandao ya kijamii imezimwa hii leo nchini Uganda wakati wa zoezi muhimu la kuchagua Rais pamoja na wabunge wa kuwawakilisha wananchi.

Rais wa nchi hiyo Yoweri Musevrni amenukuliwa akisema kuwa mitandao hoyo imezimwa kwa lengo jema la kuzuia kusambaza taarifa za uongo na za kichochezi ambazo zinaweza kusababisha matatizo katika taifa hilo.

Kituo kimoja cha uchaguzi uchaguzi wake umesitishwa jijini Kampala baada ya kutokea kutoelewana baina ya wananchi na askari waliokuwa wakilinda amani na usalama.

Aidha Mgombea Urais Dkt. Kiza Besgye amesema haamini kama uchaguzi huo utakuwa huru na haki kuanzia upigaji kura hadi upatikanaji wa matokeo.
Chanzo BBC