
Mtoto mdogo, Gindu Kilulu mwenye umri wa miaka 6 aliyekuwa amembeba pia mtoto mwenzake mgongoni, amenusurika kuuawa na fisi baada ya kumvamia saa 2 asubuhi wakati akimpeleka mtoto mwenzake huyo kwa mama yake aliyekuwa akikamua maziwa.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Lupakisyo Andrea Mjukuu wa Kapange, amesema Serikali haitambakisha fisi yoyote atakayetokea kushambulia binadamu.