
Mbunge wa Kawe Josephat Gwajima, alivyowasili kwenye viwanja vya Bunge kuitikia wito wa Spika Job Ndugai
Mbunge huyo wa Kawe Askofu Josephat Gwajima, amechukua hatua hiyo alivyowasili kwenye viwanja vya Bunge hii leo kwa ajili ya kuhojiwa mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili kujibu tuhuma mbalimbali zinazomkabili, ambapo aliomba kubadilishiwa vitu hivyo.
Mbunge Gwajima aliwasili kwenye viwanja vya Bunge Jijini Dodoma majira ya saa 6:40 mchana kwa ajili ya kuhojiwa ikiwa ni kuitikia wito wa Spika wa Bunge Job Ndugai alioutoa Agosti 21 mwaka huu, ambapo pia kabla ya mahojiano aliomba pia msaidizi wake amletee dawa zake anywe.
Askofu Gwajima alitakiwa kufika mbele ya kamati hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 4 (1) (a) na (b) ya nyongeza ya nane ya kanuni za kudumu za Bunge toleo la Juni 2020 ambayo inaipa mamlaka kamati hiyo kuchunguza mambo yanayohusu maadili ya wabunge yanayopelekwa kwa Spika.