Kaimu Kamanda Mkuu wa kikosi Cha Trafiki Tanzania, SACP Fortunatus Musilimu
Kamanda Musilimu amesema kwamba kama jeshi la polisi, ulinzi na usalama barabarani hawataweza kuendelea kushuhudia ajali nyingi zikiendelea barabarani kutokana na madereva wazembe, hivyo watahakikisha maadhamio waliyoyapanga yanatekelezwa kwa asilia zote.
"Tutakuwa wakali sana kwa madereva wazembe, Hatutawachapa kwa viboko maana hakuna sheria inayosema hivyo. Lakini adhabu tutakazokuwa tukizitoa ni sawa na adhabu ya viboko. Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Naibu Waziri Wa Mambo ya Ndani Massauni alisema inabidi kuchukua hatua kali dhidi ya madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani, ikibidi hata kuwachapa viboko akimaanisha adhabu na sivyo kama watu walivyomnukuu", Musilimu alifafanua
